Wednesday, June 3, 2009

Shughuli ya Hitima ya Marehemu Nassoro Makuka


Shughuli ya Hitima ina utaratibu wake na inakusanya watu wa aina mbalimbali wazee kwa vijana, wake kwa waume na watoto pia. Hivi karibuni nilihudhuria hitima ya marehemu Nassoro Makuka jirani yangu tuliyeishi naye kijijini Kisemvule. Hitima hiyo ilifanyika nyumbani kwao kitongojini Mpera si mbali sana kutoka Kisemvule. Watu walifurika kwa wingi. Licha ya mvua kubwa iliyonyesha siku hiyo, shughuli ya hitima ilikwenda vizuri sana. Sala iliendeshwa na mashehe nguli baada ya hapo sadaka ilitolewa. Mpangilio mzuri wa kugawa chakula ulifanyika bila bugudha. Pichani umati wa watu wakiwa tayari kupata sadaka. Mungu aiweke pema roho ya marehemu Nassoro bin Makuka.
Amina

No comments: