Saturday, June 27, 2009

Kujiamini na kujituma siri ya ushindi wa USA dhidi ya Hispania

Ni wachache waliotabiri kuwa USA itashinda dhidi ya Hispania katika mashindano ya FIFA kombe la mabara mchezo wa nusu fainali uliofanyika nchini Afrika Kusini tarehe 25 Juni 2009.

Wakicheza kwa kujiamini, kujituma na uzalendo wa hali ya juu. USA iliweza kuitandika Hispania mabingwa wa Ulaya bao 2-0 mbele ya wachezaji wenye majina (mafathers) akina Fernando Torres na Ikker Cassilas anayesemekana kuwa ni mmoja wa magolikipa bora kabisa ulimwenguni. Soka ndivyo ilivyo na mpira siku zote unadunda. Walicheza kama timu na hawakujali kuwa wanacheza na wachezaji wenye majina makubwa. Lakini walikuwa na kitu cha ziada kuwa ni Waamerika taifa kubwa ingawa soka kwao ndo kwanza linapanda chati.

No comments: