Monday, June 8, 2009

Mkoa wa Singida fursa bwelele


Kwa mtazamo wa wengi mkoa wa Singida ni mkoa wenye shida na usio na maendeleo. Wafanyakazi wanapopangiwa kufanya kazi kwenye mkoa hiuo hujiuliza mara mbili mbili niende au nisiende. Sababu ni nyingi lakini si za msingi hata kidogo. Wakati mwingine ni maneno ya vijiweni- aaa mwanangu Singida choka mbaya! Ndo vijana wanavyoita. Blog hii ilipokuwa Singida hivi karibuni ilikuta mambo tofauti kabisa. Singida ni mji mzuri tu barabara zake za mji wa Singida kwa sasa zinaboreshwa kwa kuwekwa rangi. Kuna majumba mazuri kabisa karibu na ziwa Singida. Kuna sehemu mbalimbali za burudani. Hivyo vijana msisite kufanya kazi Singida mbona mambo mazuri tu na fursa bwelelee. Kikubwa ukiishi Singida huwezi kupata Cholestrol kwani alizeti ni kwa wingi - Singida mkoa wa alizeti! Pichani jengo la Mkuu wa Mkoa Singida

No comments: