Saturday, June 27, 2009

BURIAN MICHAEL JACKSON

Watu hufa na sote tutakufa. Lakini wanapokufa watu kama akina Michael Jackson dunia nzima inapata habari na hisia ni kwa watu wengi. Mwanamuziki huyu alikuwa na kipaji cha pekee katika nyanja za muziki tangu utoto wake. Alivutia watu wengi wa mataifa mbalimbali ndiyo maana kifo chake ni habari kubwa. Amefanya mambo mengi.

Hata hivyo pamoja na kuwa maarufu amepita katika misukosuko mingi ya kuchafuliwa jina lake na hata kushitakiwa. Ameacha watoto lakini hatujui kama ameacha mjane. Huyu ndiye Michael Jackson ninayemfahamu. Burian Michael.

No comments: