Saturday, June 27, 2009

Hivi tumejitayarisha kwa bei mpya za mafuta

Ni majuzi tu tulipokuwa tukifurahia kushuka kwa bei za mafuta na hata kushuka gharama za usafirishaji. Lakini ghafla bei zimepanda tena. Hii ina maana kuwa gharama za usafirishaji zitaongezeka na kusababisha kupanda kwa gharama za maisha. Bei za mafuta zimeongezeka wakati Bunge la Bajeti linaendelea huko Dodoma. Kama Bajeti hizi zilitayarishwa kwa bei za chini za mafuta kwa vyovyote vile utekelezaji wa mipango yetu kwa kiasi kikubwa itaathirika. Ndiyo maana nauliza je tumejitayarisha kwa bei mpya za mafuta?

No comments: