Tuesday, June 23, 2009

Wamiliki wa mabus wanapokuwa na sauti dhidi ya abiria

Kabla ya kutangazwa nauli mpya za mabus kutokana na kushuka kwa bei za mafuta. Usafiri kutoka Mbagala R3 hadi Kisemvule haukuwa na matatizo. Mabus yalikuwa yanapatikana wakati wote na nauli ilikuwa sh 600 kwa mtu mzima. Mara tu bei ziliposhuka na kuwa sh 400. Wamiliki wa mabus wamekuwa wakipeleka mabus kwa kupenda wao tena kwa nauli ya si chini ya sh 500. Hii maana yake nini? Utakuta abiria wamejazana pale Mbagala R3 lakini mabus yanakwenda Mkuranga. Hayataki kupakiza watu wa Vikindu wala Kisemvule. SUMATRA mko wapi? Hivi ni halali kwa wenye mabus kuwanyanyasa abiria kwa hali hii?

No comments: