Thursday, August 19, 2010

Cocacola na DAWASCO katika KILIMO KWANZA



Maonyesho ya NaneNane ya mwaka 2010 katika viwanja vya Mwl.J.K.Nyerere mkoani Morogoro yameleta mengi ya kujifunza kwa yale tusiyoyafahamu. Blog hii ilipata bahati ya kutembelea banda la Idara ya Mipango ya MATUMIZI bORA YA ardhi ya Kilimo na Hifadhi imeweza kuwashirikisha wakulima kutoka Tarafa ya Matombo, kata ya Kibungo Juu wanaoshiriki katika Mradi wa 'Equitable Payments for Watershed Services (EPWS) - Tanzania unaowezeshwa na CARE International-Tanzania kuonyesha teknolijia wanazotumia katika kuhifadhi ardhi ya milima ya Uluguru ambayo ni chanzo kikuu cha mto Ruvu ambao maji yake hutumiwa na wadau mbalimbali kama vile Kampuni ya CoCaCola na DAWASCO. Kampuni hizi kwa kupitia mikataba maalumu kati yao na vikundi vya wakulima huwalipa wakulima katika jitahada zao za kuhifadhi ardhi na vyanzo vya maji. Hapa ndipo ile dhana ya 'Public Private Partnership'katika kilimo inapojionyesha katika uhalisia wake.

No comments: