Wednesday, August 4, 2010

Kocha Poulsen amrudisha Kaseja Taifa Stars


Kocha mpya wa Taifa Stars Mdenish Jan Poulsen amemrudisha Juma Kaseja katika kikosi cha Taifa Stars. Kaseja anaaminika kuwa ni golikipa nambari moja kwa sasa nchini Tanzania, hata kwa kipindi kirefu sasa hajaonekana langoni akiichezea Taifa Stars kwa kile kilichodaiwa na kocha wa zamani Maxio Maximo kuwa ni mtovu wa nidhamu.Hii ni nafasi pekee kwa Kaseja kuwadhihirishia Watanzania kuwa haikuwa kweli, na inampasa kujituma ili aweze kupata namba ya kudumu katika Taifa Stars.

No comments: