Wednesday, August 4, 2010

Utaratibu mzuri wa kupanda mabus ya wanafunzi unahitajiwa


NDIYO, Bank ya CRDB imetoa mabus machache kwa ajili ya wanafunzi wa jiji la Dar Es Salaam. Pamoja na kuwa na mabus hayo bado wanafunzi hugombania wakati wa kupanda mabus hayo. Kwanini kusiwepo utaratibu mzuri wa kuingia kwenye mabus hayo? Njia rahisi ni kwa wanafunzi kujipanga katika mstari. Aliyewahi ndiye atakuwa wa kwanza kupanda gari. Wanafunzi mkifanya hivi hata abiria wengine wataiga kwenye vituo vya mabus. Mnapogombania bus kuna hatari ya kuchana sare zenu za shule, kuchafuka, kuibiwa, kuchana vitabu na madaftari na wakati mwingine hata kuumia na kuzua ugomvi usio na sababu.

No comments: