Thursday, September 2, 2010

Inabidi kutulia na kutafakari pia


Bado tunaendelea na Warsha ya Habari na Mawasiliano katika Kilimo hapa jijini Pretoria Afrika ya Kusini. Leo ni siku ya nne kuna mambo mengi sana niliyojifunza lakini pia nimechangia mengi katika warsha hii na bado naendelea kuchangia mpaka kieleweke. Kikubwa si kuwasiliana tu bali mawasiliano yanasaidia nini katika uzalishaji wa kilimo hatimaye kuboresha maisha ya wananchi katika eneo hili la kusini mwa Afrika? Inabidi kutulia na kutafakari kwa kina.

No comments: