Tuesday, January 31, 2012

Maktaba ya Chuo cha Uhasibu Arusha

Nikiwa Jijini Arusha jengo hili lilinisisimua. Lakini nilipoambiwa kuwa ni maktaba ya chuo nilifurahishwa sana. Unapokuwa na jengo zuri la Maktaba kama hili chuoni jua kwamba waliobuni chuo hicho walikuwa wanauelewa mpana kuhusu Elimu. Chuo kisichokuwa na maktaba iliyokamalika basi kina dosari. Maktaba hii ni ya kisasa huenda ikawa ni moja kati ya maktaba bora zaidi hapa nchini. Nimeshatembelea vyuo vingi, taasisi nyingi za serikali na zisizo za kiserikali sijaona maktaba nzuri kama hii. Hata lile jengo la Maktaba Kuu ya Taifa- Barabara ya Bibi Titi jijini Dar Es Salaam haifui dafu na hili! Kwenye blog hii niliwahi pia kupost Maktaba ya Mkoa wa Arusha bure kabisa! Tuamke kila mkoa, taasisi mbalimbali hasa shule kuanzia nursery hadi vyuo vikuu vianze kuboresha au kujenga maktaba za kisasa ambazo zitakuwa visima vya maarifa.

No comments: