Friday, December 30, 2011

Nawatakia kila la Kheri mwaka mpya 2012


Leo Ijumaa ni siku yangu ya mwisho ya kazi hapa ofisini kwa mwaka huu wa 2011. Mwaka huu umekuwa na milima na mabonde katika maisha yangu. Kuna wakati nililia sana hasa mwezi huu wa 12 na kuna wakati nilifurahi sana.Mwaka 2011 nimeshughulika na kusafiri sana kwa shughuli za kikazi. Sikukosa katika masuala ya jamii katika familia yangu kwenye kikundi chetu cha Africana pia nilikuwa kwenye mstari wa mbele kushiriki katika masuala ya dini hasa katika Parokia yangu ya Vikindu.Hata hivyo kuhusu blog ni mwaka wa mafanikio. Nimeweza kuvunja rekodi ya miaka iliyopita nimening'iniza 476!. Mwezi ambao sikufanya vizuri ulikuwa ni mwezi Septemba. Nawashukuru wadau wote wa Banzi wa Moro. Kupitia blog hii watu wamefahamiana, wameshauriana na kupata vitu vipya.NAWATAKIA MWAKA MPYA WENYE MAFANIKIO

No comments: