Tuesday, July 3, 2012

Amewahi kikaoni


Watanzania tuna tabia isiyoridhisha ambayo inatakiwa tujirekebishe haraka sana. Tabia ya kuchelewa kwenye mkutano,sherehe, kazini siyo tabia nzuri. Utakuta wachache wamewahi lakini wengi huchelewa tena inawezekana hata zaidi ya masaa mawili! Pichani Dada Ghana Kunambi kushoto amewahi,akiwa na mwenyeji wa kikao cha Africana Dada Editruda nyumbani kwake Buguruni.Wengine wako wapi? Kwa Dar Es Salaam kama umeambiwa kikao ni saa 6.00 mchana anza kusafiri kuanzia saa 4.00. Ni heri kuwahi kuliko kuchelewa. Dar vurugu ni nyingi, traffic jams pia kuna weza kutokea tukio ambalo hukulitegemea likakuchelewesha. Kumbuka sababu na samahani nyingi sana mara nyingi haziwasaidie wengine sana sana unaendelea kupoteza muda tu. Kumbuka kuchelewa ni gharama!

No comments: