Monday, July 30, 2012

Mbolea kwenye rambo ! Haiwezekani

Ndivyo alivyokuta CEO wa Tanzania Fertilizer Regulatory Agency Dkt. Suzana Ikerra wakati wa ukaguzi wa maduka yanayouza mbolea mkoani Ruvuma. Kuna sehemu alikuta mbolea imefungwa kwenye vifuko vidogo vyepesi na vyeusi vya rambo. Wauzaji wakidai wanauza mbolea ya 'Sulphate of Ammonia' (SA)! Hii haiwezekani hata kidogo mbolea kuuzwa kwenye mifuko ya rambo. Kuna athari nyingi kwa kufanya hivyo baya zaidi hata wakulima hawana uhakika na bidhaa wanayouziwa matokeo yake mbolea hiyo ikitumiwa mashambani inaweza kutoa matokeo yasiyotarajiwa kama vile kuunguza mimea.

No comments: