Tuesday, July 31, 2012

Uncle God Kyando Luhungu

Tarehe 28/7/2012 kwetu Kisemvule tulitembelewa na mgeni maarufu si mwingine ni uncle God Kyando Luhungu anayeishi Kurasini jijini Dar. God, ni mtoto wa dada yangu marehemu Averina Constantine Gega (Mrs A.Luhungu) a.k.a Dada Ave aliyefariki siku chache baada ya kuzaliwa God.God sasa yuko darasa la sita. Ingawa amevalia T-shirt ya kijani (pichani) yeye ni mpenzi mkubwa wa klabu ya Simba (mnyama) kwa hapa nyumbani na ni shabiki wa Chelsea huku majuu!.Angalia jinsi anavyofuatilia matangazo ya mechi ya Yanga na Azam iliyochezwa tarehe 28/7/2012 kupitia kiredio kidogo ambapo Yanga iliibuka mshindi na kunyakua Kombe la Kagame kwa kuibamiza Azam 2-0. Uncle God pamoja na mimi mjomba wake (Mwanachama wa Simba) hatukufurahia hata kidogo ushindi huo wa Yanga!

No comments: