Tuesday, July 31, 2012

Tunapokuwa Bungeni Dodoma

Tunapowakilisha Bajeti zetu Bungeni- Dodoma si lele mama. Kazi kubwa ni kujibu hoja za wabunge. Mwezi Julai 2012 Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika iliwasilisha Bajeti yake na hivi ndivyo wataalamu walivyojitayarisha kujibu hoja zilizoibuliwa na wabunge.
Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo Dkt. F.Myaka (mwenye laptop)akiwa katika ukumbi wa Kilimo IV Dodoma
Wataalamu wa kilimo wakifuatilia kwa makini mawasilisho ya Bajeti ya Wizara kupitia luninga wakiwa ndani ya jengo la Kilimo IV Dodoma
Kuna hoja zilizoumiza vichwa lakini zilijibiwa na hatimaye bajeti ikapita.

No comments: