Wednesday, August 28, 2013

Bidhaa za wajasiriamali wetu

Nilifurahi nilipoona wajasiriamali wengi waliojitokeza kwenye maonyesho ya wakulima yaliyofanyika kitaifa kule Dodoma mapema mwezi agosti 2013.Wanawake walikuwa mstari wa mbele kuonyesha ubunifu wao. Kwenye banda hili Banzi wa Moro aliweza kununua mkoba mdogo wa kuweka vifaa vya wanafunzi kwa bei ya Tshs 10,000/=. Hakika mkoba huo sasa anautumia mmoja wa mabinti zangu na anaupenda sana kuliko mikoba ya mtumba!

No comments: