Wednesday, August 28, 2013

Zabibu kutoka Makutopora

Zabibu aina ya Makutopora kutoka kituo cha Utafiti-Makutupora, Dodoma ni moja ya matunda ya watafiti wetu wa Tanzania. Zabibu hizi zinafaa kutengenezwa mvinyo mweupe na hasa champaigne ni tamu pia zikitafunwa. Kinachotakiwa kwa sasa ni kusambaza aina hii ya mbegu kwa wakulima wa zabibu na pia kuboresha viwanda vyetu vya kuzalisha mvinyo. Kwanini tuagize champaigne kutoka nje? Aina hii ya zabibu inapaswa kupigiwa debe. Watanzania tupende vya kwetu!

No comments: