Friday, August 30, 2013

Wanachama wa RESEWO

Tarehe 29/08/2013 Kikundi cha wataalamu kutoka Wizara ya Kilimo chakula na Ushirika walioko kwenye mafunzo ya juma moja yanayohusu jinsia katika shughuli za kilimo kilitembelea kikundi cha wajasiriamali kiitwacho RESEWO (Regent Estate Senior Women Group)kinachoundwa na akinamama wapatao 22 wengi wao wakiwa wastaafu waliojikita katika uzalishaji wa mboga za asili kama vile mnavu,mchicha maua,delega na mazao mengine.Kikundi hiki kinafanya mambo mengi na wanayo mengi ya kueleza kuhusu mboga na mimea ya asili tuliyonayo ambayo wengi hutafahamu. Wanapatikana katika Kijiji cha Makumbusho, kando ya barabara ya Ali Hassan Mwinyi, katika Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar Es Salaam.Watemblee.

No comments: