Tuesday, March 3, 2009

Kilimo bora ni pamoja na usafiri wa uhakika


Tunapozungumzia kilimo bora si mbolea pekee wala si maji pekee wala si mbegu tu na pengine si matrekta. Kilimo bora ni pamoja na kuwa na usafiri wa kusafirisha mazao kutoka shambani hadi ghalani, kiwandani au sokoni.


Zao la chai ni moja ya zao linalohitaji usafiri wa uhakika na wa haraka mara tu chai inapovunwa kutoka shambani kwenda kiwandani ili itayarishwe kuwa majani ya chai. Bila ya kuwa na usafiri wa uhakika chai huharibika. Hii huwa ni hasara kwa mkulima. Kwani chai ya mkulima inakuwa na thamani inapofika kiwandani kwa wakati. Hivyo basi ni muhimu wakati tunapozungumzia kilimo tuwe na muono mpana. Pichani wakulima wakipakia chai katika lori maalumu lilitengenezwa kusoma chai kutoka mashambani.

No comments: