Wednesday, March 4, 2009

Tanzania inayo nafasi nzuri ya kuzalisha mpunga


Hali ya uzalishaji wa mazao ya nafaka duniani kwa sasa si nzuri.Uzalishaji umeshuka sana na bei ya mazao ya nafaka kwa nchi nyingi duniani inazidi kupanda.


Mwenendo huu ingawa siyo mzuri, lakini unaipa nafasi Tanzania kuzalisha zaidi mazao ya nafaka kwani soko lipo. Moja ya mazao ambayo Tanzania tunaweza kuzalisha kwa wingi na kuweza kujitosheleza kwa chakula na kuweza kupata soko nchi nyingine ni zao la mpunga.


Tanzania tuna ardhi ya kutosha, vyanzo vingi vya maji na hata utaalamu upo. Kinachotakiwa ni juhudi za kusudi ili kuweza kutumia fursa iliyopo. Watanzania tubadilike fursa zipo tuzitumie. Wenzetu k.m.Amerika asilimia 5% ya wananchi wanaojishughulisha na kilimo wanalisha asilimia 95% na kuuza ziada. Tanzania asilimia 85 ni wakulima lakini wanashindwa kulisha asilimia 15 ambayo haijishughulishi na kilimo? Kwa mwenendo huu hatuwezi kuendelea hata kidogo.

No comments: