Tuesday, March 3, 2009

PRRR.. KUMBE NI MKENYA

Jana nilikuwa nikiangalia kipindi kimoja cha mahojiano katika NTV hapa Nairobi. Ni mahojiano na moja wa magwiji wa sanaa nchini maarufu kwa jina la "papa shilandula" baadaye nilikuja kugundua kuwa huyu ndiye aliyeshiriki kwenye tangazo la cocacola la PRRR linaloonyeshwa kwenye TV.

Msanii huyu kwa kweli ana kipaji. Kwanza anaongea kwa mantiki anajua anachokifanya na anategemea nini. Nilichojifunza kwake ni kuwa hana makeke. Hata gari lake ni la kawaida kabisa. Ni kipande cha baba kweli. Hata kiingereza chake ni safi sana. Mahojiano yale yalikuwa mazuri sana. Wasanii wetu wanaweza kujifunza kutoka kwa "papa shilandula" (jina la kisanii).

No comments: