Tuesday, March 3, 2009

Mfumo wa Kupelemba na Kutathmini uwe na meno


Wataalamu wa Kupelemba na Kutathmini wanaoendelea na warsha iliyoandaliwa na ASARECA hapa Nairobi Kenya katika mada zao wamesisitiza kuwa wakati umefika wa kuweka mfumo wa M&E wenye meno. Wakiwa na maana kuwa ikiwa mambo hayaendi kama yalivyopangwa katika shughuli za utafiti lazima hatua zichukuliwe. Kwa mfano hakuna sababu ya kuendelea na utafiti ambao unaonekana dhahiri kuwa hautakuwa na mafanikio.


Hakuna sababu ya kuwa tafiti mpya kila mwaka kama hakuna umuhimu wa tafiti hizo. Aidha hakuna haja ya kuwa na mtafiti mzembe! Hata hivyo wametahadharisha kuwa M&E siyo polisi. Lakini ni mfumo wa kutoa ushauri ya nini kifanyike ili kilete mafanikio yaliyokusudiwa.

No comments: