Friday, March 13, 2009

Precision Air wameweza

Hakuna ubabaishaji, uswahili na nini sijui. Precision Air inafanya vitu vya uhakika. Tarehe 1/3/2009 nilisafiri kwenda Nairobi Kenya na kurudi tarehe 7/3/2009 kwa kutumia Precision Air. Tuliondoka kwa wakati muafaka na tulirudi kwa wakati muafaka. Huwezi kuamini tulifika Dar saa 8.00 kama ilivyoandikwa kwenye tiketi huduma ndani ya ndege safi kabisa lugha nzuri na vijana wachangamfu. Kampuni hii ya ndege ni kioo bora cha nchi yetu katika usafiri wa anga ipewe ushirikiano unaostahili. Jamani Precision Air siyo tu wanaweza, wameweza.

No comments: