Friday, March 13, 2009

Samaki hawa wangeweza kujenga sekondari

Hadi jana zaidi ya tani 90 za samaki zilikuwa zimeshapakuliwa kutoka kwenye meli iliyokamatwa ikivua samaki katika bahari ya Hindi eneo la Tanzania. Katika taarifa ya habari iliyorushwa na TBC 1 ilieleza kuwa inakisiwa kuwa inawezekana kuwa bado kuna tani 90 na zaidi. Wamekuta pia mayai ya papa na mashavu yake ambayo yana thamani kubwa huko Asia.

Ina maana miaka zaidi ya arobaini tulikuwa tunaibiwa hivi hivi. Huku tukiendelea kuwa masikini. Samaki peke yake wangeweza kujenga shule za msingi na sekondari zilizo bora na kuongeza maslahi ya walimu. Hivi miaka yote hiyo hatukujua kuwa tunaibiwa? au kuna wenzetu walikuwa wanakula nao? Hii ni zaidi ya EPA. Hongera Magufuli umepanda chati haraka sana kwa hili.

No comments: