Wednesday, March 25, 2009

Kwa Joseph ni zaidi ya Ubwabwa


Watoto hupenda kula wali au ubwabwa. Hata sisi tulipokuwa watoto na hata leo bado tunapenda kula wali. Tulipokuwa tukisoma sekondari siku ya kula wali kila mmoja alikuwa msafi kwenda bwaloni. Na mgawaji alikuwa anapiga nyengo kwa wengine na kujipendelea mwenyewe kwa kujaza sahani yake. Kweli wali ni mtamu hasa na maharage. Ni chakula kinachopendwa na wengi hasa hapa Tanzania. Pichani uncle Joseph Julius akibugia ubwabwa kwa jazba!

No comments: