Monday, March 2, 2009

Iwapo tutakwepa kodi nchi haiwezi kuendelea


Watanzania wengi hawalipi kodi.Hawaoni umuhimu wa kulipa kodi lakini wanataka maendeleo. Wanalamikia kiwango duni cha elimu, huduma duni ya afya, barabara mbovu, haduma za umeme na maji zisizo ridhisha. Hii ni mifano tu ya huduma zinazoweza kuboreshwa iwapo kodi zinazohusika zitalipwa.Tukilipa kodi serikali inaweza kuaagiza matrekata madogo (pichani) yatakayowarahisishia wakulima wetu shughuli za shamba.

Tunanunua vitu madukani lakini hatupewi stakabadhi.Wafanyabiashara wengi wanakwepa kodi tena za mabilioni. Kwa mwendo huu tutaweza kuwalipa walimu wetu mishahara mizuri, madaktari wetu na wafanyakazi wengine. Watanzania wenzangu tulipe kodi kwa maendeleo yetu na maisha bora.

No comments: