Thursday, April 3, 2014

Duka la Mzee Moris wa Kiswira -Matombo

Miaka ya sitini na sabini kijijini kwetu maduka yalikuwa yanahesabika. Hili ni duka la Mzee Moris Martin. Mtoto wa Akida Martin. Hapa tuliweza kununua sukari, chumvi,viberiti  na vinginevyo. Duka hili lilikuwa kijijini Kiswira Matombo, Morogoro karibu kabisa na Kanisa Katoliki Parokia ya Matombo. Kwa sasa duka hilo halina bidhaa tena. Kijijini Kiswira maduka sasa ni mengi  na bidhaaa mbalimbali zinapatikana kama zinavyopatikana mjini Morogoro.Kweli wakati ukuta.

No comments: