Friday, April 4, 2014

Nguvu ya Jua yasukuma maji Kisemvule-Mkuranga




Asilimia kubwa ya nchi yetu ya Tanzania inapata mwanga wa jua kwa muda mrefu kwa siku. Mwanga huu ukitumiwa vizuri kwa kuzingatia teknolojia zilizopo zinazoendeshwa kwa nguvu ya juu utasaidia sana kuboresha maendeleo ya watu wetu vijijini. Nguvu ya jua (solar power) inaweza kusukuma pump za maji, kutoa umeme kwa matumizi ya nyumbani  na hata viwanda vidogovidogo. Miaka ya hivi karibuni Shirika lisilo la Kiserikali  la African Reflections kutoka Marekani  limekuwa likichimba visima vya maji katika mkoa wa Pwani hasa wilaya ya Mkuranga. Pichani mtaalamu akifunga panel ya solar kijijini Kisemvule itakayotumika kutoa nguvu ya kusukuma pump ya maji ya kisima. Kinachotakiwa ni utunzaji wa  miundo mbinu hiyo. Kwa kutumia solar power wananchi watapata huduma ya maji wakati wowote. Hii itapunguza kwa kiasi kikubwa gharama ya kulipia bill ya umeme wa TANESCO.

1 comment:

Unknown said...

mama cat na mzee pembe wale