Friday, April 4, 2014

Msongamano wa magari barabara za Mandela na Kilimo jijini Dar

Hapa ni makutano ya barabara ya Kilimo na Nelson Mandela karibu kabisa na yalipo makao makuu ya  Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika wilayani Temeke eneo la Veterinary. Kuanzia saa nane hadi 12.30 jioni kila siku kwenye makutano haya mpaka mpale TAZARA  kunakuwa na msongamano wa magari. Hivi hakuna utaratibu wa kuyafanya magari yanayotoka Bandari kutumia barabara ya Mandela kwa masaa maalumu? Je ni nani aliyempa  Mamlaka mmiliki wa Kampuni ya Magari ya Dandho kuweka malori yake kwenye barabara ya Kilimo na kuwafanya Wafanyakazi wa Kilimo kukosa amani katika kufanya kazi wakibugudhiwa na kelele za magari hayo na msongamano?

No comments: