Thursday, February 7, 2013

Aliyeiua Cameroon

Huyu ndiye Mbwana Samata (aliyemiliki mpira) aliyeiua Cameroon jana kwenye uwanja wa Taifa. Siku zote ninasema hakuna kisichowezekana na si kweli kuwa nchi nyingine za Kiafrika hata dunia zinatupita sana kiuchezaji. Tatizo tulikuwa hatujajipanga, hatujitambui na hatujiamini. Sasa tumeanza kujipanga, tunajitambua,tunajiamini. Na ndiyo maana katika kipindi kifupi tumeweza kuzifunga Zambia na Cameroon zinazosemekana kuwa ni vigogo wa soka barani Afrika. Ndiyo, tuanze sasa kuvaa sare za akina Mbwana Samata, Frank Dumayo, Juma Kaseja na wengine. T
uwatangaze wachezaji wetu na kutangaza soka la Tanzania.

No comments: