Thursday, February 7, 2013

Mboga kutoka bonde la Chang'ombe

Kwa miaka mingi bonde la Chang'ombe limekuwa likistawisha aina mbalimbali za mboga zikiwemo bamia, mboga za mabgoa, na mchicha. Wakazi wengi wa Jiji la Dar Es Salaam hutegemea bonde la Chang'ombe kwa mboga. Halmashauri ya Manispaa ya Temeke ikiandaa Mpango Mkakati wa Kilimo mzuri wa jinsi ya kulitumia bonde hilo kwa shughuli za bustani mabadiliko makubwa ya uzalishaji wa mboga zilizo na ubora na uwingi wa kutosha kwa matumizi ya wakazi wa jiji la Dar utapatikana. Hii pia itawaongezea kipato wazalishaji wa mazao ya bustani katika bonde hilo.

No comments: