Thursday, February 7, 2013

Hapa ndipo 'Kempski'

Siku za kazi wakati wa mchana ukinipigia na nikakujibu kuwa niko 'Kempsiki' basi ni hapa.Ukiwa 'Kempsiki' unapata vyakula vya leoleo. Kuanzia samaki aina ya changu,kibua pamoja na mboga za maboga, tembele, kisamvu, bamia na maharage, nyama za kukaanga, wali kwa nazi na ugali wa kuviringwa. Huduma zake ni poa pia hapa hakuna daraja! Bei zake pia ni kivutio cha wateja. 'Kempsiki' inapatikana karibu kabisa na yalipo Makao Makuu ya Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika wailaya ya Temeke, maeneo ya Veterinary ni jirani pia na ofisi za usafirishaji ya Kampuni ya DANDHO.

No comments: