Sunday, April 21, 2013

Kanisa Kuu la Mt. Paulo wa Msalaba-Dodoma

Leo kwa mara ya kwanza nimesali katika kanisa hili la Mt.Paulo wa Msalaba-mjini Dodoma.Ni kanisa kubwa na zuri. Ibada iliendeshwa kwa lugha ya Kiingereza. Kwaya iliongozwa na Wasichana wa Shule ya Sekondari (Sikuuliza jina la shule). Baada ya misa Masista wa kutoka Parokia ya Kristu Mfalme jimbo Kuu la Dar Es Salaam walipata fursa ya kujitangaza na kuwaomba wasichana wenye sifa kujiunga na shirika lao la kitawa. Sifa ni msichana aliyemaliza kuanzia darasa la saba na kuendelea. Shirika hilo limejikita zaidi katika masuala ya elimu na tiba.

No comments: