Monday, March 9, 2015

Miwa ya kutafuna

Hapa ni Kingolwira, Morogoro. Miwa inauzwa. Hii ni miwa ya kutafuna. Kuna aina mbili za miwa.Moja ni ile ya kutafuna na ile inayotumika kutengeneza sukari. Kwa kawaida miwa ya kutengeneza sukari ni miyembamba na migumu. Miwa ya kutafuna ni laini. Hii imenikumbusha wakati nikisoma shule ya msingi nyumbani Matombo wakati wa mapumziko wanafunzi tulikuwa tukitafuna miwa kwa sana tu hadi matumbo kujaa maji mengi ukikimbia yanalia-kubwakubwkubwakubwa. Ha Moro ina kila kitu.

No comments: