Monday, March 9, 2015

Iliyokuwa Abood Soap Industries-Moro


Hapa ni Msamvu Morogoro, ndipo kilipokuwa kiwanda cha kutengeneza sabuni za 'Abood Soap'. Sabuni hizi zilikuwa maarufu si kwa Moro tu bali nchi nzima. Utengenezaji wa sabuni hizi umesitishwa miaka mingi iliyopita. Kilichobaki ni majengo na sidhani kama mitambo bado ipo (sijaingia ndani ya kiwanda). Abood mwenyewe sijui anasema nini kuhusu kiwanda chake. Wakazi wa Moro waliokuwa wakifanya kazi kwenye kiwanda hiki sasa hawana ajira kwa hiyo familia zilizokuwa zikitegemea kiwanda hiki kwa kipato zimeathirika sana.

No comments: