Monday, February 23, 2015

Kuongeza thamani ya mazao yetu isiishie mdomoni




Maabara zina vifaa vya kawaida kabisa na visivyo na gharama kubwa, hata hivyo taasisi za utafiti wa kilimo nchini India zinafanya utafiti wa uhakika kuhusu uongezaji thamani ya mazao na teknolojia baada ya mavuno (post-harvest technologies). Timu ya wataalamu wa kilimo na Mifugo iliyofanya ziara ya mafunzo nchini India mwaka 2014 iliweza kutembelea maabara hizo na kujionea wenyewe jinsi utafiti wa kuongeza ubora wa mazao unavyofanyika kuanzia mpunga hadi matunda. Tulipata bahati ya kuonja juisi iliyo kwenye utafiti. Mambo yakienda sawa kampuni mmoja itazalisha kwa wingi juisi aina hiyo hivyo mtafiti,kiwanda,wafanyabiashara na walaji kunufaika. Wadau hao wanaweza kuchangia utafiti wa uzalishaji na usindikaji wa matunda hayo.

No comments: