Monday, February 23, 2015

Fanya yako- Ujumbe mzito

Leo asubuhi wakati nikija kazini nakumbana na ujumbe  mzito  'fanya yako' ulioandikwa kwenye gari  la miguu mitatu  aina ya PIAGGIO. Nilitafakari. Ni ujumbe mzito.Nikakumbuka kuwa kwenye mkoba wangu kuna Camera nikaipiga picha.Muwasilishaji anaweza kuwa sahihi au hapana. Ndiyo usipofanya yako nani atakufanyia. Lakini upande mwingine je furaha unayoipata au karaha unayoipata ni kwa kufanya yaliyo yako peke yake? Tafakari.

No comments: