Monday, February 2, 2015

Wakulima wa Skimu ya Umwagiliaji ya Mlali-Morogoro


Hii ni skimu ya umwagiliaji ya Mlali mkoani Morogoro. Si mbali sana kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe. Wakulima wa Skimu hii wamepata mafunzo ya kilimo bora cha mpunga kutoka mradi wa wa EAAPP kuanzia mwaka 2012. Uzalishaji katika skimu hii sasa umeongezeka kutoka uzalishaji wa magunia 18 hadi kufikia 30 kwa ekari. Mwezi Januari ni wakati wa kaanda mashamba ndiyo hali tuliyoikuta kwenye skimu hiyo.
Kwa kupitia vyanzo vingine vya fedha, wakulima wa skimu ya Mlali wamejengewa ghala ya mazao. Hii itawasaidia wakulima kuhifadhi mazao yao na pia kuyauza kwa bei yenye faida.

No comments: