Tuesday, February 10, 2015

Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika




Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika lilikutana mjini Morogoro kuanzia tarehe 26-27 Januari 2015 ni kikao cha pili tangu Baraza jipya liundwe, lakini ni kikao cha kwanza kwa mwaka 2015. Masuala mengi yalijadiliwa pamoja na Mada mbalimbali kuwasilishwa zikiwemo zile zilizohusu masuala ya Mifuko ya Jamii, Bajeti ya Wizara, Majukumu ya Wajumbe wa Baraza, UKIMWI na Magonjwa Sugu Yasiyoambukizwa  na Maadili ya Utumishi wa Umma. Wajumbe walikuwa na hoja kemkem kutokana na mada zilizowasilishwa, ufafanuzi ulitolewa na maazimio ya kutekelezwa yaliainishwa.

No comments: