Monday, February 23, 2015

Tuache siasa tufanye utafiti





Sayansi lazima itumike na utafiti lazima ufanyike ili kuweza kukabiliana na matatizo katika nyanja mbalimbali. Katika kilimo matumizi ya bioteknolojia hasa ya Genetic Modified Organisms nchi nyingine imekuwa vigumu kukubalika. Tulipokuwa India tulitembelea Taasisi inayoshughulikia masuala ya bioteknolojia. Binafsi nilishangaa kuwakuta watafiti wengi vijana wakijihusisha na fani hiyo na wengi wao ni wanawake. Maabara zao zimejaa vifaa na madawa ya kufanyia utafiti ndiyo maana vijana wanavutiwa na fani hii. Hata hapa Tanzania, maabara yetu ya bioteknolojia iliyopo Mikocheni  watafiti waliowengi ni vijana. Tuache siasa tufanye utafiti na kuwekeza katika utafiti.

No comments: