Tuesday, February 10, 2015

Tuwekeze kwenye utafiti





Kutatua matatizo ya kilimo shambani hatuna budi kuwekeza kwenye utafiti. Hivi ni vifaa vichache kwenye maabara ya udongo nchini India ambavyo vinatumika katika uchunguzi wa udongo.

Kabla ya kuwekeza kwenye uzalishaji wa mazao lazima hali ya udongo ifahamike ili kuweza kutambua aina ya zao linalotakiwa kustawishwa. Hapa Tanzania maabara za udongo ziko chache sana. Ile ya Kitaifa iko Mlingano, Tanga nyingine Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine-Morogoro, Ukiriguru-Mwanza, Selian-Arusha na Uyole-Mbeya.Vifaa vya maabara ya udongo kama ilivyo kwa maabara ya magonjwa ya binadamu, ni ghali mno! Hata hivyo ni muhimu kuwa navyo kama kweli tunataka kuwekeza kwenye kilimo cha kisasa. Hali ilivyo kwenye maabara zetu nyingi si nzuri. Tunao watafiti waliobobea lakini wanakosa vifaa vya kisasa vya kuendesha utafiti wao, ndiyo maana wakati mwingine wadau wanalalamika kuwa ukipeleka sampuli yako ya udongo pale Mlingano-Tanga inachukua muda mrefu kupata majibu.

No comments: