Monday, March 23, 2015

Peter Massawe - Daktari bingwa wa Vipando vya korosho

Sekta ya kilimo kuna madaktari bingwa waliobobea katika fani mbalimbali. Mmojawapo ni Dkt.Peter Massawe-Daktari Bingwa wa Vipando (Plant Breeder) aliyebobea katika zao la korosho. Massawe ni Mratibu wa Utafiti wa Taifa wa zao la korosho. Utafiti wa zao la korosho hapa nchini unaratibiwa katika kituo cha Utafiti cha Naliendele kilichopo mkoani Mtwara chini ya Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Idara ya Utafiti na Maendeleo. Mwaka huu  Kamati ya Taifa ya Mbegu imeidhinisha aina 24 za mbegu bora korosho chotara zilizotafitiwa na watafiti wa zao hilo chini ya uongozi wa Dkt.Massawe. Hongera Dkt. Massawe na timu yako.

No comments: