Monday, March 8, 2010

Eti debe la viazi ni shilingi 2500/=


Blog ya Mjengwa leo imejaa picha za mazao yanayouzwa kwa bei ya kutupwa huko Makambako Iringa. Debe la viazi mviringo linauzwa kwa bei ya shilingi 2500/= . Maana yake ili aweze kununua bati moja itambidi auze madebe yasiyopungua sita. Madebe 180 ya viazi ndiyo yanayotosheleza kununua mabati 30 yanayotosho kuezeka nyumba ndogo.Katika hali hii si rahisi kukipenda kilimo.

No comments: