Wednesday, March 3, 2010

Tulikula mananasi


Wakulima wadogowadogo wanailisha Tanzania. Miezi mitatu iliyopita ilikuwa miezi ya mananasi. Jiji la Dar lilitapakaa kwa mananasi. Bahati mbaya mengi yalioza kwa kukosa teknolojia za kuhifadhi matunda au za kuongeza thamani.

Wakulima walio wengi wanalima kwa mazoea, wanalima kwa kubahatisha. Kilimo hapa Tanzania hakilipi sana. Miundo mbinu ni mibovu. Hakuna mitandao mizuri ya kuwawezesha wakulima kupata mikopo. Bila mikopo kilimo hakina faida. Huwezi kulima zaidi ya ekari mbili!

No comments: