Saturday, March 20, 2010

MUNGU MPELEMBAJI NA MTATHMINI No 1

Nipo hapa Pretoria- Afrika ya Kusini kwa muda wa siku tano sasa nikipata msasa katika taaluma ya Kupelemba na Kutathmini Shirikikishi (Participatory Monitoring and Evaluation). Mafunzo haya yameandaliwa na SADC . Washiriki ni wadau kutoka katika nchi zinazounda SADC (South Africa haina mwakilishi. Kuna wawakilishi wawili kutoka Tanzania. Pamoja na mambo mengine nimepata kufahamu kuwa MUNGU ni Mpelembaji na Mtathmini namba moja. Kwani sisi ni wadau wake na ana nyenzo mbalimbali za kufanya hiyo kazi. Tunapopelemba na kutathmini shughuli yoyote ile lengo lake ni kukusanya taarifa zitakazotuwezesha kufahamu mwenendo wa utekelezaji wa kazi,mradi katika muda fulani kwa kuzingatia malengo tuliyojiwekea. Tunapata kutambua mafanikio na changamoto ambazo zinaweza kutusaidia katika kufanya maamuzi. Lakini shughuli ili iwe na mafanikio inabidi kushirikisha wadau hii hasa ndiyo maana ya 'Participatory'Je, wewe unayesoma blog hii una amini?

No comments: