Wednesday, March 3, 2010

Wachina na biashara ya magogo


Hivi karibuni sehemu ninayoishi mimi miembe kadhaa imeangushwa na kukatwa vipingili vidogo vidogo. Wilaya ya kilosa pia biashara ya magogo hasa ya miti ya mazao kama vile miembe na minazi imeshamiri. Na imebainika kuwa matajiri wa biashara hiyo ni Wachina. Wanavifanyia nini vigogo hivyo hatujui. Nani karuhusu biashara hiyo. Pia hatujui. Tusije kushangaa kukosa embe. Tusije kushangaa kukosa nazi. Haya yote ni ya kujitakia.

No comments: