Wednesday, March 3, 2010

Ulanga kujenga nyumba za watumishi


Hivi karibuni wilaya ya Ulanga imetangaza mpango wa kujenga nyumba 14 za watumishi ambazo zitakaliwa na familia zipatazo 28. Kwa mujibu wa Mhandisi wa ujenzi wa wilaya hiyo, Hassan Matua mkakati wa ujenzi wa nyumba hizo umekuja baada ya kubaini kuwa watumishi wa sekta mbalimbali waliokuwa wakipangiwa kufanya kazi katika wilaya hiyo kukimbia kutokana na mazingira magumu pamoja na ukosefu wa nyumba. Huu ni mfano mzuri wa kuigwa na ni kivutio kwa wafanyakazi.

No comments: