Tuesday, February 23, 2010

Anauza mikate!


Leo asubuhi nimeinyaka picha hii kutoka kwenye blog ya ndugu yangu Mjengwa. Picha hii imepigwa Zanzibar. Mfanyabiashara huyu raha mustarehe anauza mikate kwenye tenga huku akiitangaza waziwazi bila kufunikwa. Usalama wa afya za walaji je. Hata huku Tanzania Bara tabia hii ya wafanyabiashara kutojali usalama wa afya za walaji ni tatizo sugu. Utaona samaki wa kukaanga wanauzwa barabarani bila kuhifadhiwa, korosho zimewekwa kwenye mafungu na kuguswaguswa na wanunuzi. Hii kwa kweli si tabia nzuri. Wafanyabiashara wajifunze utaratibu mzuri wa kuuza bidhaa zao hasa vyakula.

No comments: