Monday, February 22, 2010

Kisu kimenolewa acha kabisa mchezo


Ndiyo, baada ya kukaa muda mrefu kwa maumivu, Ulimboka Mwakingwe 'Uli' amerudi na makali mapya dimbani kwenye kikosi cha Wekundu wa Msimbazi (SSC). Kasi imeongezeka na shabaha ya goli kama kawa! Kuna nini tena mbona kazi kwisha. Ubingwa ni dhahiri mwaka huu. Pichani Uli katika kasi yake akimtoka Stephen Mwasika wa Moro United katika mchezo wa ligi kuu uwanja wa UHURU hapo jana (21/02/2009). Simba ilishinda kwa magoli 4-1. Picha kwa hisani ya gazeti la Mwananchi.

No comments: